Wednesday, October 30, 2013

RAIS WA CAF AMPONGEZA MALINZI

JAMALI  MALINZI



Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF), Issa Hayatou amempongeza Jamal Malinzi kwa kuchaguliwa kuwa Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) katika uchaguzi uliofanyika Oktoba 27 mwaka huu.

Katika salamu zake kwa niaba ya Kamati ya Utendaji ya CAF na familia ya mpira wa miguu Afrika, Rais Hayatou amesema uchaguzi huo unampa Rais Malinzi fursa ya kuupeleka mbele mpira wa miguu nchini Tanzania.

Amesema CAF ina imani uwezo wake katika uongozi, uzoefu na ujuzi katika mpira wa miguu havitausaidia mpira wa miguu Tanzania pekee bali Afrika kwa ujumla, na kuongeza kuwa ataendeleza ushirikiano uliopo ili kuwanufaisha zaidi vijana wa bara hili.

Rais Hayatou amemtakia Rais Malinzi kila la kheri katika kipindi chake cha uongozi na kumhakikishia kuwa CAF iko pamoja naye katika kusukuma mbele gurudumu la kuendeleza mpira wa miguu.

PAMBANO LA YANGA, MGAMBO SHOOTING LAINGIZA MIL 37/-
Pambano la Ligi Kuu ya Vodacom kati ya Yanga na Mgambo Shooting lililochezwa jana (Oktoba 29 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam limeingiza sh. 37,915,000.

Washabiki waliohudhuria mechi hiyo namba 46 iliyomalizika kwa Yanga kuibuka na ushindi wa mabao 3-0 walikuwa 6,515 ambapo viingilio vilikuwa sh. 5,000, sh. 8,000, sh. 15,000 na sh. 20,000.

Mgawo wa mapato hayo ulikuwa kama ifuatavyo; Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) sh. 5,783,644.07, gharama za kuchapa tiketi sh. 3,145,790 wakati kila klabu ilipata sh. 8,550,741.95.

Wamiliki wa uwanja walipata sh. 4,347,834.89, gharama za mchezo sh. 2,608,700.93, Bodi ya Ligi sh. 2,608,700.93, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 1,304,350.47, Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 1,014,494.81.

SIMBA, KAGERA SUGAR KUUMANA KESHO
Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) inaanza raundi ya 12 kesho (Oktoba 31 mwaka huu kwa mechi kati ya Simba na Kagera Sugar itakayofanyika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 10 kamili jioni.

Viingilio katika mechi hiyo itakayooneshwa moja kwa moja na Azam Tv kupitia TBC 1 vitakuwa sh. 5,000, sh. 8,000, sh. 15,000 na sh. 20,000 kwa VIP A.

Nayo Yanga itashuka uwanjani Novemba Mosi mwaka huu katika mechi nyingine ya ligi hiyo dhidi ya JKT Ruvu itakayochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Novemba 2 mwaka huu kutakuwa na mechi nne; Mgambo Shooting na Coastal Union (Uwanja wa Mkwakwani, Tanga), Tanzania Prisons na Oljoro JKT (Uwanja wa Sokoine, Mbeya), Azam na Ruvu Shooting (Azam Complex, Dar es Salaam), na Mtibwa Sugar na Rhino Rangers (Uwanja wa Manungu, Morogoro).

Raundi hiyo itakamilika Novemba 3 mwaka huu kwa mechi moja ambapo Mbeya City itakuwa mwenyeji wa Ashanti United kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya.

Mechi za kukamilisha mzunguko wa kwanza wa ligi hiyo zitachezwa Novemba 6 na 7 mwaka huu. Novemba 6 ni JKT Ruvu vs Coastal Union, Ashani United vs Simba, Kagera Sugar vs Mgambo Shooting, Rhino Rangers vs Tanzania Prisons na Ruvu Shooting vs Mtibwa Sugar.

Novemba 7 mwaka huu, Azam itacheza na Mbeya City wakati Yanga itacheza na Oljoro JKT kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Boniface Wambura Mgoyo
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

COLE KUTOONDOKA CHELSEA MPAKA MKATABA WAKE KUMALIZIKA


Chelsea defender Ashley Cole is eager to stay at the club beyond the end of his current contract at Stamford Bridge.
The 32-year-old's deal with Jose Mourinho's side is due to expire at the end of the season.
Cole has enjoyed great success since joining Chelsea from Arsenal in 2006, winning one Premier League title, four FA Cups and the UEFA Champions League.
"I signed an extension at the start of the year and so have this year left and it will be up at the end of the season," Cole told The London Evening Standard.
"I hope to stay for longer. I have had a great time here, a great career here and, of course, I’d love to stay if they still want me.


Tuesday, October 29, 2013

BREAKING NEWS! AJALI YATOKEA MLIMA WA MZALENDO IGAWILO JIJINI MBEYA KUELEKEA DAR ES SALAAM.





 LORI BAADA YA KUDONDOKA

 HILI NDILO TERA LILILO DONDOKA


TASWIRA YA MJI WA IRINGA KWA SASA ,HII NI KUPISHA ZIARA YA MAKAMU WA RAIS ANAYETOKEA NJOMBE







HALI  ILIVYO KWA SASA  MJI  WA IRINGA BAADA YA  POLISI  KUZUIA  MAGARI  YOTE  KATIKA  BARABARA  KUU  KUSUBIRI  MSAFARA  WA MAKAMU  WA RAIS WA TANZANIA  KUPITA  KUTOKA  MKOANI NJOMBE AMBAKO AMEKWENDA  JANA  KATIKA MAZISHI  YA ASKOFU MSTAAFU  WA RC NJOMBE

PICHA GARI LILILOBEBA SHEHENA YA MBOLEA LAPATA AJALI ISYONJE TUKUYU MBEYA, WANANCHI WAONDOKA NA MIFUKO YOTE YA MBOLEA.

Gari lenye namba T319BCU upande wa nyuma na Kichwa namba T885 CBS  aina ya Roli likiwa limepinduka

 Mbolea ikiwa imemwagika

 Gari lenye namba T319BCU upande wa nyuma na Kichwa namba T885 CBS  aina ya Roli upande wa mbele baada ya kupata ajali

 Wakazi Mbalimbali wakiwa wanashuhudia ajali hiyo

 Hii ndio Mbolea ambayo wananchi wameondoka  nayo yote


Hili ni eneo Jirani na ajali ilipo tokea

Monday, October 28, 2013

MAPUNDA AITWA NA KIM



KOCHA wa timu ya soka ya Tanzania, Taifa Stars, Kim Poulsen, amemwita kipa wa zamani wa timu hiyo, Ivo Mapunda, katika kikosi cha pili cha timu hiyo kwa ajili ya michuano ya Chalenji itakayofanyika mwezi ujao mjini Nairobi, Kenya.

Mapunda anayecheza soka ya kulipwa katika Klabu ya Gor Mahia ya Kenya, anamweka nje kipa namba moja wa Taifa Stars, Juma Kasema, ambaye tangu amalize mkataba wake na Simba amekuwa hana timu ya kuchezea.

Kipa huyo ameitwa katika kikosi cha pili cha Stars kilichopewa jina la Future Young Taifa Stars, kitakachoingia kambini Novemba 9, kinachojumuisha nyota 30, wakiwamo wawili kutoka timu ngeni katika Ligi Kuu ya Bara, Mbeya City ya Mbeya, ambapo watakaofanya vizuri watapandishwa hadi kikosi cha Stars.

Nyota waliomo kwenye kikosi hicho ambacho Novemba 13 kitacheza mechi ya kirafiki dhidi ya Taifa Stars; Makipa: Aishi Manula (Azam), Hussein Shariff (Mtibwa Sugar) na Ivo Mapunda (Gor Mahia, Kenya).

Mabeki: David Luhende (Yanga), Hassan Mwasapili na John Kabanda (Mbeya City), Himid Mao , Said Morad, Wazir Salum na Ismail Gambo (Azam), Issa Rashid, Miraji Adam (Simba), Kessy Khamis (Mtibwa Sugar), Michael Pius (Ruvu Shooting) na Mohamed Hussein (Kagera Sugar).

Viungo: Amri Kiemba, Ramadhani Singano, Haruna Chanongo, Jonas Mkude na William Luccian (Simba), Farid Mussa, Khamis Mcha (Azam), , Hassan Dilunga (Ruvu Shooting), Simon Msuva (Yanga),

Washambuliaji: Elias Maguli (Ruvu Shooting), Hussein Javu (Yanga), Joseph Kimwaga (Azam), Juma Liuzio (Mtibwa Sugar), Mwagane Yeya na Paul Nonga (Mbeya City).

Kim alisema kuelekea mechi hiyo ya kirafiki, Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager itaingia kambini Novemba 12 kabla ya siku itakayofuata kucheza na Future Young Taifa Stars kuelekea michuano ya Kombe la Chalenji.

Baada ya mechi hiyo, kambi ya Future Young Taifa Stars itavunjwa na kubaki Stars itakayoondoka Novemba 14 kwenda Arusha kwa kambi na kucheza mechi ya kirafiki ya kimataifa kabla ya kwenda Nairobi, Kenya kwa ajili ya michuano ya Kombe la Chalenji itakayopigwa kuanzia Novemba 27 - Desemba 12.

Nyota 16 wa Taifa Stars na timu zao kwenye mabano ambao wataingia kambini Novemba 12, ni Ally Mustafa (Yanga), Mwadini Ali (Azam), Aggrey Morris (Azam), Kelvin Yondani (Yanga), Shomari Kapombe (AC Cannes, Ufaransa) na Nadir Haroub (Yanga).

Erasto Nyoni (Azam), Vincent Barnabas (Mtibwa Sugar), Salum Abubakar (Azam), Mwinyi Kazimoto (Markhiya, Qatar), Frank Domayo (Yanga), Athuman Idd (Yanga), Mrisho Ngasa (Yanga), Thomas Ulimwengu (TP Mazembe, DRC), Mbwana Samata (TP Mazembe, DRC) na John Bocco (Azam).

Wachezaji wengine kumi kutoka Future Young Taifa Stars baadaye wataongezwa katika kikosi kitakachounda timu ya Tanzania Bara (Kilimanjaro Stars) kwa ajili ya michuano ya Kombe la Chalenji.


YANGA, MGAMBO JKT KUMENYANA TAIFA LEO


MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu ya Bara leo itashuka katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kupambana na Mgambo JKT katika mchezo wa raundi ya kumi na moja ya ligi hiyo.
Yanga inaingia uwanjani leo ikiwa na pointi 19 ilizopata katika mechi 10 ilizocheza huku ikiwa nafasi ya nne. Azam inaongoza ligi hiyo ikiwa na pointi 23 ikifuatiwa na Simba yenye pointi 20 huku zote zikiwa zimecheza mechi 10. Mbeya City ni ya tatu ikiwa na pointi 20 katika mechi 10.
Kwa upande wao, Mgambo wanaingai uwanjani wakiwa na pointi tano walizopata katika mechi 10. Timu hiyo inaburuza mkia katika ligi hiyo.
Kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya leo kutakuwa mchezo utakaozikutanisha timu mwenyeji za mkoa huo ambazo ni Mbeya City na Tanzania Prisons. Rhino Rangers na JKT Ruvu zitacheza katika Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mjini Tabora.

Raundi ya 12 ya ligi hiyo itaanza Oktoba 31 mwaka huu kwa mechi kati ya Simba na Kagera Sugar kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam wakati Novemba Mosi mwaka huu kutakuwa na mechi kati ya Yanga na JKT Ruvu kwenye uwanja huo huo.
Novemba 2 mwaka huu kutakuwa na mechi nne; Mgambo Shooting na Coastal Union (Uwanja wa Mkwakwani, Tanga), Tanzania Prisons na Oljoro JKT (Uwanja wa Sokoine, Mbeya), Azam na Ruvu Shooting (Azam Complex, Dar es Salaam), na Mtibwa Sugar na Rhino Rangers (Uwanja wa Manungu, Morogoro).
Raundi hiyo itakamilika Novemba 3 mwaka huu kwa mechi moja ambapo Mbeya City itakuwa mwenyeji wa Ashanti United kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya.
Mechi za kukamilisha mzunguko wa kwanza wa ligi hiyo zitachezwa Novemba 6 na 7 mwaka huu. Novemba 6 ni JKT Ruvu vs Coastal Union, Ashani United vs Simba, Kagera Sugar vs Mgambo Shooting, Rhino Rangers vs Tanzania Prisons na Ruvu Shooting vs Mtibwa Sugar.
Novemba 7 mwaka huu, Azam itacheza na Mbeya City wakati Yanga itacheza na Oljoro JKT kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.


Tuesday, October 22, 2013

INIESTA MBIYONI KUSAINI MKATABA MPYA BARCELONA



Andres Iniesta is close to signing a new five-year contract with Barcelona, the club's vice-president has revealed.
The Spain international midfielder - whose current deal expires in June 2015 - had reportedly been stalling on a new contract.
Iniesta, 29, was linked with a move away from Camp Nou, with Manchester United and Manchester City among those said to be interested in his services.

Saturday, October 19, 2013

PICHA MBALI MBALI ZA MATUKIO KATIKA UZINDUZI WA MKOA WA NJOMBE



Rais Jakaya Mrisho Kikwete akibofya kitufe huku wazee wa Njombe wakirusha njiwa kuashiria kuzinduliwa rasmi mkoa wa Njombe leo Oktoba 18, 2013 katika Uwanja wa Sabasaba mjini Njombe


Burudani ikiendelea kwa ngoma ya asili toka Ludewa kutumbuiza.

 Picha/ mchoro unaoonesha jinsi kitakavyokuwa kituo cha mabasi kikikamilika kujengwa huko Mjimwema.



                                      


FILIKUNJOMBE AWALAUMU WENZAKE WA CCM KWENYE MCHAKATO WA KATIBA MPYA.




Akihojiwa na shirika la utangazaji (BBC) kuhusu mchakato wa katiba unavyokwenda, Filikunjombe amewalaumu wabunge wenzake wa CCM kwa kuutumia wingi wao vibaya na hivyo kushindwa kuwawakilisha vema wananchi.

Pia Filikunjombe amewaonya wabunge wa CCM kuacha kumpotosha Rais katika utendaji wake kwa kuitumia vibaya demokrasia ya "wengi wape"

Thursday, October 17, 2013

TANZANIA NA RWANDA NCHI ZENYE UTAWALA BORA ZAIDI EAC



Arusha, Oktoba 17, 2013 (EANA)– Tasisi ya Mo Ibrahim juu ya Utawala Bora Afrika, imebaini nchi za Rwanda na Tanzania kuwa nchi zenye utawala bora zaidi katika Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) kati ya nchi 52 za kiafrika.

Kwa mujibu wa ripoti iliyotolewa Jumatatu, Rwanda imepata wastani wa asilimia 57.8 ikiwa ni zaidi ya wastani wa kiafrika wa asilimia 51.6.
Hii inamaanisha kwamba nchi hiyo imeboresha utawala bora kwa zaidi ya asilimia 10.9 tangu mwaka 2000, ikiwa nafasi ya kwanza kwa nchi za Afrika mashariki ikifuatiwa na Tanzania iliyoshika nafasi ya 17 barani Afrika kwa kupata asilimia 56.9 huku Uganda ikiwa ya tatu ECA kwa kuwa ya 18 kwa kupata asilimia 56. Kenya imekuwa ya 21 na kushika nafasi ya nne kwa kupata asilimia 53.6 huku Burundi iliyopata asilimia 43.8 ikishika nafasi tano kwa EAC.
”Rwanda imekuwa ikifanya vizuri mwaka hadi mwaka tangu mwaka 2000, ikiwa ni maboresho makubwa zaidi katika nyanja ya Maendeleo ya Binadamu hususa ni katika sekta ya elimu na afya,” ripote ilisema.
Mauritania imeshika nafasi ya kwanza katika Afrika kwa kupata asilimia 82.9 ikifuatiwa na Botswana aliyopata asilimia 77.6 ambapo Cape Verde imeshika nafasi ya tatu kwa kupata asilimia 76.7. barani.
Ripoti hiyo imebaini kwamba asilimia 94 ya nchi za Afrika ikiwemo Rwanda watu wake wanaishi katika nchi ambazo zimeboresha kwa ujumla masuala ya utawala bora tangu mwaka 2000.
Asilimia sita ya watu wanaoishi kwenye nchi ambazo kiwango cha utawala bora kimeshuka tangu mwaka 2000 ni pamoja na nchi za Guinea-Bissau, Madagascar, Somalia, Libya na Mali.
Taasisi hiyo ya Mo Ibrahim pia hutoa tuzo kwa viongozi bora barani Afrika.Hata hivyo tuzo hiyo haijatolewa kwa mara ya nne sasa.
Tuzo hiyo hotolewa kwa kiongozi wa Afrika aliyechaguliwa kidemokrasia aliyeonesha kwa vitendo uongozi bora,kutumikia muhula wake wa uongozi na kuachia ngazi miaka mitatu iliyopita.

TANZANIA YASAINI MIKATABA MITANO NA CHINA



SERIKALI ya Tanzania imeasaini mikataba ya makubaliano (MoUs) mitano ambayo itasadia kutoa fursa za biashara, mafunzo na masuala ya sayansi na teknolojia kwa Watanzania.
Mikataba hiyo imetiwa saini leo jioni (Alhamisi, Oktoba 17, 2013) mbele ya Waziri Mkuu Mizengo Pinda na Waziri Mkuu wa China, Mhe. Li Keqiang mara baada ya viongozi hao kufanya mazungumzo rasmi ya Kiserikali jijini Beijing, China.
Mikataba hiyo ni Mkataba wa Ushirikiano baina ya Tanzania na China kwenye masuala ya Sayansi na Teknolojia; Mkataba wa Kuruhusu bidhaa za baharini ziweze kuuzwa China; Mkataba wa Ushirikiano baina ya Tanzania na China kwenye masuala ya Utalii. Mingine ni Mkataba wa Makubaliano baina ya Tanzania na China wa kuanzisha Ukanda wa Kisasa wa viwanda vya nguo pamoja na kukuza zao la pamba na wa mwisho ni mkataba wa kutoa vitalu namba 60 na 61 kwa ajili ya ujenzi wa ubalozi wa China jijini Dar es Salaam.
Katika mazungumzo yao, Waziri Mkuu ambaye yuko katika siku ya pili ya ziara ya kikazi yake ya siku tisa kwa mwaliko wa Serikali ya nchi hiyo, alimweleza Waziri Mkuu wa China kwamba anaishukuru Seriklai ya nchi hiyo kwa misaada mbalimbali ambayo China imekuwa ikiitoa kwa Tanzania.
“Tunaishukuru kwa misaada mbalimbali na mikopo ambayo imekuwa ikitolewa kwa masharti nafuu ikilinganishwa na mikopo ya kibiashara ambayo hutolewa na nchi nyingine na kawaida ina gharama kubwa kwa Taifa,” alisema Waziri Mkuu wakati akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kumaliza mazungumzo na mwenyeji wake.
Alisema alitumia fursa hiyo kusisitiza uwekezaji kwenye sekta za kilimo, nishati, elimu na miundombinu hasa reli, bandari na teknohama. Kwenye kilimo, Waziri Mkuu alikumbusha suala la upatikanani wa soko kwa zao la tumbaku lakini akaomba uwepo umuhimu wa pekee kwa wawekezaji wa viwanda vya kusindika korosho katika mikoa ya kusini.
“Katika ziara yangu nitapenda kusisitiza haja ya uwekezaji kwenye zao la korosho… nitazungumza na maafisa wanaohusika ili tuone jinsi ya kulipa msukumo zao hili ambalo lina soko kubwa sana hapa China,” alisema.
Alimweleza Waziri Mkuu wa China dhamira ya Serikali ya Tanzania kulipa deni la dola za marekani milioni 24.6 ambalo lilitolowa kama mkopo kwa ajili ya kufufua kiwanda cha nguo cha urafiki.
“Tumeahidi kuanza kulipoa deni hilo katika mwaka wa fedha 2014/2015. Waziri wa Fedha alishaandika barua kwa Serikali ya China tangu mwezi Septemba kuonyesha nia ya Serikali ya kulipa deni hilo,” alisema Waziri Mkuu
Kesho (Ijumaa, Oktoba 18, 2013) Waziri Mkuu atafungua mafunzo ya siku 10 kwa maafisa 20 kutoka idara na taasisi za serikali za hapa nchini yanayoendeshwa kwa pamoja baina ya Chuo cha Uongozi cha China na Taasisi ya Uongozi ya Tanzania; atatembelea kiwanda cha Aluminium hapa Beijing, atakutana Bodi ya Tumbaku, Kampuni za Umeme za China Power Investment (CPI) na State Grid Corporation. Pia atakutana na kampuni ya mafuta ya CNOOC. Jioni atakutana na Watanzania waishio Beijing kwenye ubalozi wa Tanznaia nchini China.



WAWILI WAUWAWA KINYAMA MBOZI




WILAYA YA MBOZI – MAUAJI

MNAMO TAREHE 16.10.2013 MAJIRA YA SAA 22:30HRS HUKO KATIKA KIJIJI CHA MAHENJE KATA YA MYOVIZI, TARAFA IYULA, WILAYA YA MBOZI MKOA WA MBEYA.  MTU MMOJA ASIYEFAHAMIKA JINA WALA MAKAZI YAKE, JINSI YA  KIUME, UMRI KATI YA  MIAKA 20-25, ALIKUTWA AMEUAWA NA MTU/WATU WASIOFAHAMIKA KISHA  MWILI WAKE KUTUPWA KWENYE SHAMBA MALI YA  FRIDAY S/O BUKUKU.
CHANZO KINACHUNGUZWA.  MWILI WA MAREHEMU ULIKUTWA NA JERAHA UBAVU WA KULIA, UMEHIFADHIWA HOSPITALI YA WILAYA YA MBOZI. KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHNA MSAIDIZI WA POLISI DIWANI ATHUMANI  ANATOA WITO KWA YEYOTE MWENYE TAARIFA JUU YA  MTU/WATU WALIOHUSIKA KATIKA TUKIO HILI AZITOE KATIKA MAMLAKA HUSIKA ILI WAKAMATWE NA SHERIA ICHUKUE MKONDO WAKE.
WILAYA YA MBOZI – MAUAJI.
MNAMO TAREHE 16.10.2013 MAJIRA YA SAA 02:00HRS HUKO KATIKA KIJIJI CHA ISALALO, KATA YA MSIA, TARAFA YA IGAMBA WILAYA YA MBOZI MKOA WA MBEYA. TUSAMALE S/O MWILEGA, MIAKA 70, MNYIHA, MKULIMA, MKAZI WA ISALALO ALIFARIKI DUNIA AKIWA AMELALA NDANI YA  NYUMBA YAKE BAADA YA  MTU/WATU WASIOFAHAMIKA KUCHOMA MOTO NYUMBA YAKE. MAREHEMU ALIKUWA ANAISHI PEKE YAKE KATIKA NYUMBA HIYO ILIYOJENGWA KWA MATOFALI MABICHI NA KUEZEKWA KWA KUTUMIA NYASI. 
CHANZO KINACHUNGUZWA. MWILI WA MAREHEMU UMEFANYIWA UCHUNGUZI NA KUKABIDHIWA NDUGU KWA MAZISHI. KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHNA MSAIDIZI WA POLISI DIWANI ATHUMANI ANATOA WITO KWA YEYOTE WENYE TAARIFA JUU YA  MTU/WATU WALIOHUSIKA KATIKA TUKIO HILI AZITOE KATIKA MAMLAKA HUSIKA ILI WAKAMATWE NA SHERIA ICHUKUE MKONDO WAKE.
Signed by: 
[DIWANI ATHUMANI - ACP] 
KAMANDA MKOA MBEYA.

Wednesday, October 16, 2013

VIINGILIO MECHI KATI YA YANGA NA SIMBA VYAWEKWA HADHARANI




KIINGILIO cha chini kwenye mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kati ya Simba na Yanga itakayochezwa Jumamosi ya Oktoba 18 mwaka huu kitakuwa sh. 5,000. Kiingilio hicho ni kwa viti vya rangi ya kijani ambavyo ni 19,648.
 
Kwa upande wa viti vya rangi ya bluu kiingilio ni sh. 7,000, viti vya rangi ya chungwa itakuwa sh. 10,000, VIP C kiingilio ni sh. 15,000, VIP B itakuwa sh. 20,000 wakati VIP A yenye viti 748 tu tiketi moja itapatikana kwa sh. 30,000. 
 
Tiketi zitaanza kuuzwa siku moja kabla ya mchezo huo utakaoanza saa 10 kamili jioni katika vituo mbalimbali. Vituo hivyo ni Shule ya Sekondari Benjamin Mkapa, Sokoni Kariakoo, mgahawa wa Steers ulioko mtaa wa Ohio/Samora, Oilcom Ubungo, Kituo cha Mafuta Buguruni, Dar Live Mbagala, Uwanja wa Uhuru, na BMM Salon iliyoko Sinza Madukani.
 
Mechi hiyo namba 63 itachezeshwa na Israel Nkongo kutoka Dar es Salaam, ambapo atasaidiwa na Hamis Changwalu wa Dar es Salaam pia, na Ferdinand Chacha wa Bukoba. Mwamuzi wa akiba ni Oden Mbaga wa Dar es Salaam.
 
Kamishna wa mechi hiyo atakuwa John Kiteve kutoka Iringa wakati mtathmini wa waamuzi (referees assessor) ni Stanley Lugenge wa Njombe.
 
MECHI TATU FDL ZASOGEZWA MBELE
Mechi tatu za Ligi Daraja la Kwanza (FDL) katika kundi A na C zimesogezwa mbele kutokana na viwanja vya Kambarage, Shinyanga na Nangwanda Sijaona, Mtwara kuwa na shughuli nyingine za kijamii.
 
Katika kundi A, mechi kati ya Ndanda na Transit Camp iliyokuwa ichezwe Oktoba 19 mwaka huu sasa itafanyika Oktoba 21 mwaka huu kwenye Uwanja wa Nangwanda Sijaona.
 
Stand United na JKT Kanembwa zilizokuwa zicheze Oktoba 19 mwaka huu, sasa mechi hiyo ya kundi C itafanyika Novemba 2 mwaka huu Uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga. Nayo mechi ya Mwadui na Polisi Dodoma iliyokuwa ichezwe kwenye uwanja huo Oktoba 26 mwaka huu imesogezwa hadi Novemba 3 mwaka huu.

 *Imeandaliwa na Boniface Wambura Mgoyo, Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

Sunday, October 13, 2013

Saturday, October 12, 2013

BREAKING NEWZ-- mtangazaji wa ITV apigwa risasi


Mtangazaji wa ITV, Ufoo Saro, amepigwa risasi muda mfupi uliopita na kujeruhiwa vibaya. Hivi sasa yuko hospitali ambako anapatiwa matibabu.

Mtu aliyempiga risasi alijiua hapo hapo baada ya kuwa amemuua mama aliyekuwepo wakati wa tukio. Taarifa za awali zinasema aliyeuawa ni mama yake Ufoo Saro.

COTE D'IVORY 3 SENEGAL 1


Didier Drogba and Solomon Kalou

Ivory Coast are on course to qualify for the FIFA World Cup after a 3-1 first leg play-off victory over Senegal in Abidjan on Saturday.
Captain Didier Drogba opened the scoring with a penalty in the fifth minute for the winners, and an own goal from Lamine Sane shortly after doubled their advantage.
Salomon Kalou coolly slotted a third just after half-time for the winners, and although Papiss Cisse netted an injury-time strike for the losers, Ivory Coast still won well.
They now have the upper hand in their bid to secure a place at next year's showpiece in Brazil, with Senegal to host the second leg on November 16.
Ivory Coast coach Sabri Lamouchi made five changes to the side that drew with Morocco last time out, with Didier Zakora and Sol Bamba headlining the inclusions.
Newcastle striker Cisse – who is Senegal's leading scorer in qualification – returned to the starting line-up for the visitors as one of four changes.
The winners made the perfect start, scoring after just five minutes when Gervinho was upended by Cheikhou Kouyate in the penalty area.
Drogba sent Senegal goalkeeper Bouna Coundoul the wrong way from the spot, and things went from bad to worse for Alain Giresse's side shortly after.
The lively Gervinho, who was a constant threat for the victors, raced away down the left, before aiming at a cross at Drogba from the left.
Sane deflected the cross into his own net though, sending a partisan crowd wild as Ivory Coast led 2-0 in less than 15 minutes.
Senegal did enjoy a good spell after, posing some questions for the Ivory Coast, but Gervinho should have scored a third six minutes before the break when he raced clear and rounded Coundoul.
Gervinho's effort was blocked by Lamine Gassama though, while Yaya Toure blasted over as Ivory Coast had to be content with a two-goal lead at half time.
The third goal did arrive though, with Gervinho setting up Kalou just after the break.
The Lille striker broke the offside trap and then kept his composure, sliding past the advancing Coundoul and into the net.
Yaya Toure almost added a fourth four minutes from time when his shot flashed just past the post before Cisse gave Senegal a late lifeline.
Ivory Coast failed to deal with a long ball pumped into the penalty area and Cisse reacted quickest, smashing past goalkeeper Boubacar Barry in the fifth minute of stoppage time.
The goal gave Senegal some hope, but Ivory Coast left the pitch the happiest after a convincing win.