Wednesday, November 20, 2013

WAFUGAJI WAZUA BARA MBARALI

FAMILIA moja katika kijiji cha Utulo wilaya ya Mbarali Mkoani Mbeya imepata ulemavu wa viungo baada ya kudaiwa kupigwa na kujeruhiwa na wafugaji jamii ya kisukuma.

Akizungumzia tukio hilo mmoja wa mmoja wa wahanga aliyefahamika kwa jina la Luchina Mgaya(55) mkazi wa kijiji cha Utulo alisema wamejikuta wakiishi katika mazingira magumu baada ya kupata ulemavu hivyo kushindwa kujitafutia riziki.


FAMILIA moja katika kijiji cha Utulo wilaya ya Mbarali Mkoani hapa imepata ulemavu wa viungo baada ya kudaiwa kupigwa na kujeruhiwa na wafugaji jamii ya kisukuma.

Tukio hilo la kusikitisha liliikumba familia hiyo Januari Mwaka huu baada ya baba, Mama na mtoto kupata ulemavu baada ya kukosa matibabu yaliyotokana na kukosa msaada wa fedha kutoka kwa wanaotuhumiwa kutyenda kosa hilo.

Akizungumzia tukio hilo mmoja wa mmoja wa wahanga aliyefahamika kwa jina la Luchina Mgaya(55) mkazi wa kijiji cha Utulo alisema wamejikuta wakiishi katika mazingira magumu baada ya kupata ulemavu hivyo kushindwa kujitafutia riziki.

Luchina amesema alipigwa na wafugaji hao mapema mwaka huu baada ya mwanae wa kiume kuvamiwa na wafugaji hao wakidai kuwa aliwachongea kwenye uongozi wa kijiji hali iliyopelekea kukamatwa.

Alisema Baada ya kuona mwanae anapigwa mama huyo alifanya jitihada za kumuokoa ili asipate kipigo ndipo walipomgeukia na kumpa kipigo kikali yeye na mumewe ambapo yeye amepata ulemavu wa viungo na mumewe akiwa amepata upofu.

Luchina ametabanaisha kuwa baada ya kipigo kikali walitoa taarifa kwenye uongozi wa kijiji na Polisi Rujewa ambapo watuhumiwa walikamatwa na kufunguliwa kesi lakini wakaomba kesi hiyo waimalize nje ya mahakama jambo ambalo walikubaliana nalo.

Aliongeza kuwa Pamoja na kukubaliana suala hilo kulimaliza nje ya mahakama ambapo watuhumiwa walikiri kutenda kosa na kuahidi kulipa jumla ya shilingi laki tano ikiwa ni gharama za matibabu na shilingi milioni nne ambazo ni fidia waliahidi kulipa kwa muda wa siku mbili tu.

Mhanga huyo alisema kitu cha kushangaza ni kitendo kilichofanywa na  watu waliopewa dhamana ya kutunza amani na sheria ambao ni Mwenyekiti wa kijiji na Askari mpelezi wa kesi hiyo kuzitafuna pesa hizo na kuwaacha wahanga hawana kitu mpaka leo.

Hata hivyo baadhi ya wanaotuhumiwa kuwazunguka wahanga hao walipotafutwa kuthibitisha kutenda kosa hilo waligoma kulizumzia kwa kile walichodai hawalijui kabisa.

Aidha familia ya Luchina imekuwa ikiishi maisha ya ombaomba, pamoja na kufukuzwa katika nyumba waliyokuwa wakiishi kwa kukosa pesa  za kulipa pango la nyumba na watoto watatu wameacha masomo kutokana na kukosa ada.

Wahanga hao wameziomba taasisi mbalimbali kuwasaidia ili waweze kupata haki zao kwani wamejitahidi kufuatilia maeneo yote lakini wamekuwa wakipewa majibu ya kukatisha tamaa na wao kukata tama ya kuishi.

Kwa upande wake Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Diwani Athumani amekili kupata taarifa za tukio hilo na kuahidi kulifuatilia na kulipatia ufumbuzi ndani ya mfupi na kuongeza kuwa watakaobainika kutenda kosa hilo la kinyama watachukuliwa hatua za kinidhamu.

Vitendo vya unyanyasaji na ugomvi baina ya wafugaji na wakulima vimeendelea kuripotiwa katika maeneo mengi hapa nchini, hivyo lisipoangaliwa na kuchukuliwa kwa hatua stahiki amani ya Watanzania itakuwa matatani.

Tuesday, November 19, 2013

Rais Kikwete awasili Poland kwa ajili ya Mkutano wa Mabadiliko ya Tabia Nchi

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwasili jijini Warsaw, Poland, kuhudhuria mkutano wa Nchi wanachama wa Mkataba wa Kyoto kuhusu mabadiliko ya Tabia Nchi unaoanza leo Jumanne Novemba 19, 2013. (picha hii na zinazofuata hapo chini zimetoka Ikulu)





Sunday, November 17, 2013

CAMEROON YAISHUSHIA TUNISIA KIPIGO CHA PAKA MWIZI 4 -1


Cameroon secured their place at the FIFA World Cup finals with an emphatic 4-1 win over Tunisia on Sunday.
Volker Finke's men went into the game on the back of a 0-0 draw in the first leg in Rades last month, and knew that defeat would see them fail to qualify for only the second time since 1986.
However, the hosts were never really in danger as they produced a dominant performance to become the third African nation to reach the 2014 finals in Brazil.
Fenerbahce striker Pierre Webo opened the scoring after four minutes with a cool finish from close range.
Benjamin Moukandjo doubled Cameroon's advantage with a fine individual goal, but the home fans were given a scare when Ahmed Akaichi pulled one back for Tunisia shortly after half-time.
However, the tie was settled by Jean II Makoun, who scored a second-half brace to spark jubilant scenes at the Stade Omnisport Ahmadou Ahidjo in Yaounde.
Cameroon made three changes from the first leg, with Tottenham defender Benoit Assou-Ekotto and Nancy attacker Moukandjo among those to come in.
Fakhreddine Ben Youssef replaced Sami Allagui in attack for Ruud Krol's visitors, while defender Karim Haggui came in for Alaeddine Yahia.
It did not take the hosts long to open the scoring, Webo capitalising on some sloppy Tunisian defence with a clinical finish across Moez Ben Cherifa.
Cameroon continued to push forward in a bid to kill the tie off, and came close to doubling their lead 10 minutes later when Ben Cherifa was forced into a fine save to deny Assou-Ekotto from long range.
Finke's side were rewarded for their positivity on the half-hour mark as Moukandjo weaved past several Tunisia defenders before firing a low shot beyond Ben Cherifa to put Cameroon in command.
The visitors should have pulled one back shortly before the break, but Syam Ben Youssef headed over from point-blank range.
Tunisia did put themselves firmly back in the tie six minutes into the second half, substitute Akaichi firing home on the half-volley after breaking through the Cameroon backline.
Krol's men began to dictate proceedings following their goal, and had a claim for a penalty turned down on the hour mark after Assou-Ekotto's clumsy challenge on Fakhreddine Ben Youssef.
Just six minutes later Assou-Ekotto proved to be the creator for the goal that all but ensured Cameroon's place in the finals, Makoun heading in a pinpoint near-post corner to delight the home fans.
Moukandjo was denied his second by Ben Cherifa, but Makoun put the gloss on a superb display four minutes from time as he slotted into an empty net after Maxim Choupo-Moting had hit the post.

Saturday, November 16, 2013

Tanesco yatangaza mgao wa umeme kwa muda wa siku 10 kwenye mikoa mbalimbali na Dar ikiwemo.



Meneja Uhusiano wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) Badra Masoud amethibitisha kuwepo kwa mgao wa umeme kwenye majiji yote matano nchini pamoja na Zanzibar na mikoa mingine kadhaa kwa siku kumi kuanzia leo na kusababisha adha kwa wakazi wake.
Badra akielezea kuwa hali hiyo inayotokana na kuzimwa kwa mitambo ya kampuni ya Pan African iliyopo Songosongo alisema,“Mitambo hiyo itazimwa kwa sababu ya matengenezo ya lazima, hakuna jinsi ya kuzuia hali hiyo Tanesco tunasikitika sana kwa kuwa kutakuwa na upungufu mkubwa wa umeme kwenye gridi ya taifa,”.
Alifafanua mitambo hiyo inaendeshwa na gesi ambayo imepungua katika kisiwa hicho cha Songosongo Wilaya ya Kilwa, Lindi. “Upungufu huo umesababishwa na matengenezo ya kiufundi yanayofanywa kwenye visima vya gesi na lengo ni kuboresha upatikanaji wa gesi ya kutosha kwenye visima hivyo”.
Source : Mwananchi

LEO MAGAZETINI TAR. 16/11/2013