Saturday, November 16, 2013

Tanesco yatangaza mgao wa umeme kwa muda wa siku 10 kwenye mikoa mbalimbali na Dar ikiwemo.



Meneja Uhusiano wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) Badra Masoud amethibitisha kuwepo kwa mgao wa umeme kwenye majiji yote matano nchini pamoja na Zanzibar na mikoa mingine kadhaa kwa siku kumi kuanzia leo na kusababisha adha kwa wakazi wake.
Badra akielezea kuwa hali hiyo inayotokana na kuzimwa kwa mitambo ya kampuni ya Pan African iliyopo Songosongo alisema,“Mitambo hiyo itazimwa kwa sababu ya matengenezo ya lazima, hakuna jinsi ya kuzuia hali hiyo Tanesco tunasikitika sana kwa kuwa kutakuwa na upungufu mkubwa wa umeme kwenye gridi ya taifa,”.
Alifafanua mitambo hiyo inaendeshwa na gesi ambayo imepungua katika kisiwa hicho cha Songosongo Wilaya ya Kilwa, Lindi. “Upungufu huo umesababishwa na matengenezo ya kiufundi yanayofanywa kwenye visima vya gesi na lengo ni kuboresha upatikanaji wa gesi ya kutosha kwenye visima hivyo”.
Source : Mwananchi

LEO MAGAZETINI TAR. 16/11/2013











Thursday, November 14, 2013

TATIZO LA OMBA OMBA LAZIDI KUWA KERO JIJINI MBEYA

Mwenye tshirt nyeupe michirizi myesi akitoa maelezo kuhusu mtoto huyo


mtoto akiondoka eneo la chuo








Idadi ya Omba omba imezidi kuongezeka siku hadi siku hususani kwa miji mikubwa hapa Tanzania kama Dar es salaam, Arusha, Mwanza na Mbeya.
Hii imedhihirka jana jijini Mbeya mara baada ya mtoto mdogo kukutwa akiwa amejilaza maeneo ya chuo kikuu cha Teofilo Kisanji (old compuss). Mahojiano mafupi yalifanyika na huyo mtoto akadai baba na mama yake walishafariki hivyo anaishi katika hali ngumu kwani hana mlezi na akidai anaumwa anahitaji msaada. Baadhi ya wanachuo walimchangia kiasi cha shilingi 5000/= na wengine wakiahidi kumnunulia chakula.
Muda mfupi alijitokeza mama mmoja akasema “yule mtoto anamfaham vizuri, na ni mwongo anaishi mitaa ya mama john na wazazi wake wote wawili ila wale wazazi wanafanya kumtumia kama chambo ili wapate hela ya kujikimu kimaisha”.
Aliendelea kwa kuwataka watu kama wana moyo wakusaidia wamsaidie tuu ila sio kwamba huyu motto hana wazazi, wazazi wake wote wawili wapo na wanaishi mama john na akadai kuna kipindi walishawahi kukamatwa na polisi wakafikishwa kituoni na kuamriwa waache tabia hiyo na wafanye kazi ile wamlee vizuri mwanao.




Wednesday, November 6, 2013

CASILLAS KUBAKI REAL MADRID MPAKA MKATABA WAKE KUMALIZIKA


Real Madrid goalkeeper Iker Casillas has revealed that he intends to stay with the club until the end of his contract.
The Spain international has made just four appearances so far this season, although he played a key role in helping Real secure a 2-2 draw with Juventus in the UEFA Champions League on Tuesday.
Casillas has been out of favour since fracturing his hand in January, allowing Diego Lopez to establish himself as Real's first-choice keeper.



Milipuko nje ya ofisi za chama tawala China

Mabomu yaliyolipuliwa yalisemekana kuwa ya kutengenezwa nyumbani



Maafisa wa polisi katika eneo hilo wamesema kuwa milipuko hiyo ilisababishwa na mabomu madogo yaliyotengenewa nyumbani.
 Mlipuko huo uliotokea muda wa asubuhi wenye shughuli nyingi, ulisababisha kuvunjika kwa madirisha na moshi mkubwa kufuka.

Ripoti zilizotolewa na shirika la habari la kiserikali zilisema kuwa mabomu madogo yalikuwa yamefichwa ndani ya maua kando ya barabara.

Milipuko hiyo ilitokea Kaskazini mwa China katika eneo la, 
Tai-yuan, mkoani, Shanxi,

Taarifa za vyombo vya habari nchini humo vinasema kuwa watu 8 wamejeruhiwa na magari mawili kuharibiwa.

Picha zilizowekwa kwa mitandao ya kijamii imeonyesha moshi ukifuka pamoja na magari ya wazima moto ikiwa katika eneo la shambulizi ambalo lilitokea mapema asubuhi ya leo.

Hakuna taarifa za kina kueleza kiini cha milipuko hiyo. Hata hivyo kumekuwa ma matukio ya mara kwa mara ya wananchi kufanya mashambulizi kama haya dhidi ya serikali hasa wale ambao hawahisi kuridhishwa na serikali hiyo.

Hali ya wasiwasi pia imetanda hasa baada ya tukio la wiki jana mjini Beijing ambalo mamafisa walisema kuwa lilikuwa njama ya shambulizi la kigaidi.



SOURCE; BBC

Sunday, November 3, 2013

Bonifasi Wambura Ateuliwa Kukaimu Nafasi Angetile Osiah TFF


KAMATI ya Utendaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imemteua Bw. Boniface Wambura kuwa Kaimu Katibu Mkuu wa TFF. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na TFF kwa vyombo vya habari leo uteuzi wa Wambura unaanzia Novemba 2 mwaka huu.

Taarifa hiyo imesema aliyekuwa Katibu Mkuu wa TFF, Angetile Osiah ameagizwa kwenda likizo ya malipo hadi atakapomaliza mkataba wake kwa kipindi kilichosalia. Uamuzi huo unatolewa muda mfupi tangu uongozi mpya uingie madarakani chini ya Rais wa sasa wa TFF, Jamal Malinzi.

“Kamati ya Utendaji inaviomba vilabu, vyama vya wilaya, vyama vya mikoa, vyama shiriki na wadau wote kumpa ushirikiano Bw. Boniface Wambura katika utekelezaji wa majukumu yake.” inafafanua taarifa iliyotolewa na Malinzi, Rais mpya wa TFF.
Hata hivyo taarifa hiyo haikufafanua zaidi sababu za kumpumzisha Osiah katika nafasi hiyo akiwa ukingoni kumalizia mkataba wake wa ajira kuitumikia TFF.

TANZANIA PRISONS WAPIGISHWA KWATA NA MAAFANDE WA JKT OLJOLO SOKOINE

Timu ya tanzania prison maarufu kama wajelajela leo wamejikuta wakiambulia kichapo cha goli 1 -0 kutoka kwa maafande wenzao wa JKT Oljolo.
Iliwachukua dakika 6 tuu maafande hao wa JKT Oljolo na kuweza kuandika goli lilodumu mpaka kipenga cha mwisho cha mwamzi kinapuliza.
Tanzania prisons itabidi wajilaumu wenyewe mara baada ya 22 kuzawadiwa penalti iliyopigwa na Jeremia juma.
Tanzania prisons mara baada ya kupoteza mechi hiyo iliyopigwa uwanja wa sokoine Mbeya wameshuka mpaka nafasi ya 13 kutoka nafasi ya 12 waliyokuwepo awali.